Header Ads

LIGI YA MABIGWA ULAYA YAENDELEA LEO

 LIGI ya mabingwa Ulaya hatua ya 16 bora mtoano inatarajiwa kuanza kutimua vumbi lake leo Jumanne saa 4:45 usiku kwa michezo miwili ya mkondo wa kwanza kuchezwa katika miji ya Paris (Ufaransa) na Benfica (Ureno).

Katika mchezo wa kwanza miamba wa Hispania Barcelona wao watakuwa wageni wa Paris Saint Germain huko Parc des Princes huku Borussia Dortmund wakisafiri mpaka Ureno kwenda kuvaana na Benfica 

Kesho Jumatano michezo mingine miwili pia itachezwa ambapo mabingwa watetezi,Real Madrid watakuwa nyumbani Santiago Bernabeu kuwaalika Napoli.Bayern Munich watakuwa Allianz Arenal kupepetana na Arsenal.

Michezo mingine minne iliyosalia itachezwa wiki ijayo kabla ya kuanza kwa michezo ya mkondo wa pili.

Ratiba ya michezo ya mkondo wa kwanza

Jumanne Februari 14
Benfica v Borussia Dortmund 
Paris Saint-Germain v Barcelona 

Jumatano, Februari 15
Bayern Munich v Arsenal 
Real Madrid v Napoli 

Jumanne Februari 21 
Bayer Leverkusen v Atletico Madrid
Manchester City v Monaco

Jumatano, Februari 22
 Porto v Juventus 
Sevilla v Leicester City 

Ratiba ya michezo ya mkondo wa pili

Jumanne Machi 7
Arsenal v Bayern Munich
Napoli v Real Madrid

Jumatano Machi 8
Borussia Dortmund v Benfica 
Barcelona v Paris Saint-Germain 

Jumanne Machi 14 
Juventus v Porto 
Leicester City v Sevilla 

Jumanne Machi 15 
Atletico Madrid v Bayer Leverkusen
Monaco v Manchester City


No comments