Header Ads

N'Golo Kante mchezaji bora wa mwezi ligi kuu England chaguo la mashabiki

Kiungo wa Chelsea, N'Golo Kante ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi machi kwa kura zilizopigwa na mashabiki.

Kura 32,000 zilipigwa kupitia tovuti ya Sky Sports , huku Kante ambaye aliisaidia Chelsea kupata ushindi mara mbili mfululizo ugenini akijikusanyia kura 11,763 akiwapiku Romelu Lukaku na kiungo wa Spurs, Dele Alli.

Lukaku ambaye alifunga magoli 4 katika mechi 3 za mwezi machi amejikusanyia kura , 10,777 na Dele Alli aliyeshika nafasi ya tatu akipata kura , 4,069.

Straika wa Bournemouth, Josh King (3,114), Straika wa Leicester City, Jamie Vardy (1,290) na Winga wa Crystal Palace, Wilfried Zaha (1,251) . wakifunga idadi ya wachezaji 6.

No comments