Header Ads

SIMBA 2-1 MWADUI FC 'LIVE' MAPUMZIKO, UWANJA WA TAIFA, DAR

Dakika ya 47: Kipindi cha kwaza kimekamilika
Dakika ya 45: Mchezo unaendelea kwa kasi.
Mwadui wanapata bao la kwanza kupitia kwa Paul Nonga.
GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO
Dakika ya 40: Simba wanamiliki mpira muda mwingi, Mwadui wameanza kuwa makini zaidi na wanawabana Simba katikati ya uwanja.
Dakika ya 32: Kichuya anapata nafasi ya kupiga shuti baada ya kumzunguka beki wa Mwadui lakini shuti lake linapaa juu ya lango.
Dakika ya 30: Simba wanaendelea kulishambulia lango la Mwadui kwa nguvu, pamoja na hivyo wageni nao wanapambana kujipanga lakini wanazidiwa mbinu mara kadhaa.
Ibrahim Ajibu anaipatia Simba bao la pili, ni baada ya kupata pasi nzuri ndani ya eneo la 18, akatuliza mpira na kuutupia wavuni. Simba wana mabao mawili.
Dakika ya 26: Ajibuuuuuuu GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO
Dakika ya 19: Kichuya anaipatia Simba bao la kwanza kwa njia ya penati, alipiga upande wa kushoto, kipa wa Mwadui, Shaban Kado akaifuata lakini ikawa na kasi kubwa na kuingia ndani.
KICHUYAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA
GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO
Dakika ya 16: Simba wanapata penati baada ya Kichuya kuchezewa faulo na kipa wa Mwadui, Shaban Kado wakati akiwa ndani ya eneo la hatari.
Dakika ya 15: Simba wanashambulia lango la Mwadui, Kichuya anapata nafasi ya kupiga shuti anapiga linakuwa na nguvu ndogo na kutoka nje.
Dakika ya 10: Simba wanaendelea kupanga mipango taratibu lakini Mwadui wanakuwa makini.
Dakika ya 5: Bado mchezo haujachangamka.
Dakika ya 1: Mchezo umeanza kwa kasi ndogo.
Saa 10:00: Mwamuzi anaanzisha mchezo.

No comments