Header Ads

CECH ATWAA TUZO YA MCHEZAJI BORA

KIPA wa Arsenal,Petr Cech (Pichani) akiwa na tuzo yake mkononi baada ya kutangazwa mchezaji bora wa mwaka wa nchi ya Jamhuri ya Czech. 

Cech,35,ambaye hivi karibuni aliisaidia Arsenal kutwaa ubingwa wa kombe la FA  ametangazwa mchezaji bora kwa mara ya 11 katika kipindi cha miaka 13 iliyopita.

Cech ametwaa tuzo hiyo akiwashinda Paavel Kaderabech wa Hoffenheim na Patrik Schick Sampdoria na kufikia rekodi za wakongwe Pavel Nedved na David Lafata waliotwaa tuzo hiyo mara 11 kila mmoja.

No comments