Kiungo wa Manchester United, Paul Pogba ana uwezekano wa kuwa nje ya
uwanja kwa muda mrefu kutokana na kupata majeraha ya nyama za paja
katika mchezo wa jana dhidi ya Basel.
Pogba aliingia katika mchezo huo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa
ndiye nahodha wa timu lakini alishindwa kkuendelea katika dakika ya 19
ya mchezo huo uliopigwa kwenye Uwanja wa Old Trafford.
Alitoka na nafasi yake kuchukuliwa na Marouane Fellaini ambaye alifunga bao katika mchezo huo.
Bado hakuna jibu juu ya afya yake lakini kuna uwezekano mkubwa akawa nje ya uwanja kwa wiki kadhaa.
No comments